Logo

ibada ya jumapili

Ibada ya Jumapili

Ibada ya Jumapili katika Usharika wa KKKT Kimara ni moja na hutolewa kwa lugha ya Kiswahili.Ibada huanza saa 1:00 asubuhi na huambatana na huduma mbalimbali kama ifuatavyo:-

    • Ubatizo
    • Huduma ya ubatizo wa watoto na watu wazima hutolewa kwa mujibu wa ratiba ya kanisa.
    • Sakramenti ya meza ya Bwana
    • Hufanyika mara moja kwa mwezi.
    • Huduma hii pia hutolewa kwa wagonjwa hospitalini au nyumbani kwa utaratibu maalum.
    • Fungu la Kumi
    • Hutolewa kila Jumapili ya kwanza ya mwezi kama sehemu ya ibada.
    • Ibada ya kusifu na kuabudu
    • Hufanyika kwa utaratibu uliowekwa na Usharika kwa lengo la kukuza moyo wa ibada na sifa.
    • Ibada ya mkesha wa maombi
    • Hufanyika kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi kwa ajili ya kuomba na kuombeana.
    • Ibada ya Ndoa
    • Hufanyika kwa utaratibu unaoelekezwa na Usharika.
    • Kipindi cha Kwaresima, ibada hii haitolewi isipokuwa kwa kibali maalum.
    • Usharika pia hutoa huduma ya ndoa za pamoja kwa washarika waliokaa muda mrefu bila kubariki ndoa au waliokuwa na ndoa za serikali. Huduma hii hutolewa pale panapokuwa na mahitaji.
Karibu katika ibada ya Jumapili kwa ushirika wa kiroho, sifa, na maombi. Mungu awabariki!